Trump kufikishwa tena mahakamani

Trump kufikishwa tena mahakamani

Aliye kuwa Rais nchini Marekani, Donald Trump anatarajiwa kufikishwa mahakamani mjini Miami akikabiliwa na makosa saba yakiwemo ya kumiliki nyaraka za siri za serikali.

Aidha wakili wa trump ameweka wazi kuwa mwanasiasa huyo atafikishwa mahakamani hapo jumanne ya juni 13, 2023 lakini bado wanasubiri hati ya mashtaka.

Sambamba na hayo idara ya usalama inatarajia kukutana na wafanyakazi wa trump ikiwemo walinzi wake, leo juni 9, 2023 kwa ajili ya kupanga utaratibu wa msafara kuelekea mahakamani.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post