Vyakula vinavyoongeza urembo kwa mwanamke

Vyakula vinavyoongeza urembo kwa mwanamke

Hellow! It’s another furahi day watu wangu wa nguvu ,sasa leo nimekuja na jambo moja matata sana kwenu nyie wadada. Kama kawaida yetu kwenye kile kipengele cha fashion, kama tunavyojua kila mdada anapenda urembo wa ngozi kwa ujumla.

Basi bwana leo nimekuletea mambo ya kawaida kabisa na ni rafiki kuyapata hii sasa haina haja ya kutoa pesa nyingi ili sura yako iweze kuwa ya urembo zaidi bali ni kwa vitu na vyakula vya asili ambavyo viko karibu yako, vinavyoweza kukufanya ukawa mrembo zaidi ya watumiaji wa vipodozi vya kemikali.


Vifuatavyo ni vyakula vinavyoweza kusaidia kuimarisha afya ya ngozi:



1. Asali
Asali ambayo hutengenezwa na nyuki huwa na viambatano asilia na ni moja ya chakula muhimu kwa ajili ya kuimarisha afya ya ngozi, Asali husaidia kutunza na kuhifadhi unyevu kwenye ngozi na ina kiwango kikubwa cha sukari na asidi ambazo huzuia vijidudu wanaozaliana kwenye ngozi.


Tumia asali kwa kupaka usoni wakati unataka kwenda kuoga, kisha acha kwa muda na ioshe. Kufanya hivyo husaidia kunawirisha na kung’arisha ngozi yako.


2. Mayai
Mayai pia ni muhimu kwa afya ya ngozi yako. Kiini cha yai huwa na vitamini A na B, huku sehemu yenye ute ikiwa na protini nyingi ambayo ni muhimu pia kwa ngozi, ute wa yai ni muhimu katika kuifanya ngozi kuwa nyororo na yenye kung'aa zaidi na pia husaidia ngozi kujilinda vizuri na mionzi ya jua. 


3. Matunda
Matunda nayo ni muhimu pia hususani chungwa, parachichi na limao ambayo husaidia kuimarisha afya ya ngozi, kwa sababu husaidia kutengeneza collagen, ambayo ni aina ya protini inayotengeneza ngozi.

Ndani ya matunda hayo huwa na Vitamini C, ambayo husaidia sana kuondoa uvimbe na mikunjo ya ngozi na hivyo kuilinda ngozi isizeeke mapema.

4. Mboga za Majani
Mboga za majani pia ni muhimu kwa afya ya ngozi. Kama tujuavyo zimesheheni vitamin na virutubisho vya aina mbalimbali vyenye faida kubwa kwa ngozi na mwili kwa ujumla. Mboga hizi za majani husaidia ngozi kuzalisha seli mpya na kuondoa zile zilizokufa, hivyo kupunguza ukavu na kutunza ngozi na kuifanya ing’are na kuvutia.

5. Vyakula vya Baharini
Vyakula vya baharini kwa ujumla ni vizuri kwa afya ya ngozi. Vyakula vingi vya baharini vina kiwango kikubwa cha Zinc na Omega 3 ambazo ni muhimu kwa siha ya ngozi. Faida za Omega 3 ni pamoja na kuondoa kukakamaa au ukavu wa ngozi, kupunguza kuvimba na kukunjamana kwa ngozi na husaidia mzunguko mzuri wa damu mwilini hivyo kuboresha ngozi.

Haya sasa wewe mwanadada mfuatiliaji wa Mwananchi Scoop naatumai umepata suluhisho la ngozi yako bila hata gharama kubwa ,cha kufanya anza kupenda kula vyakula vyenye lishe bora ili uwe na ngozi bora zaidi na yenye kuvutia bila ya kupoteza pesa.

 

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post