Tweet ya Diamond yazua maswali

Tweet ya Diamond yazua maswali

Moja kati ya vitu vilivyozua maswali katika mitandao ya kijamii ni tweet ya msanii wa muziki wa kizazi kipya Nasibu Abdul maarufu kama Diamond Platnumz aliyoiweka katika ukurasa wake wa Twitter.

Msanii huyo katika ukurasa huo ameTweet kwa kusema “25 days to do……!” akiwa anamaanisha kuwa bado siku 25 ambapo amezua maswali mengi kwa mashabiki zake ambao wanataka kujua je ni kitu gani kinakuja baada ya siku hizo kuisha.

Hivi msomaji etu hata wewe unahisi kuwa ni kitu gani Diamond anatarajia kukiweka wazi baada ya siku hizo 25, usisite kututumia maoni hayo katika ukurasa wetu wa Instagram ambao ni @mwananchiscoop.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm


Latest Post