Nandy: Asante mungu kwa kunipatia best friend

Nandy: Asante mungu kwa kunipatia best friend

Weeeuuuweee! Mama wa mtoto nae hakuwa nyuma bwana naeye alizihirisha furaha yake licha ya kuzungumza kuwa watu hawatakuja kujua jinsia wala jina la mtoto wake.

Nandy kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika kuwa “Kwanza kabisa nimshukuru mungu kwa ukuu wake hakika amezaliwa binti wa kichaga.. nikisema niongee yote sitomaliza leo ila nachoweza kusema nakupenda sana mama maana nimeona umuhimu na ugumu wa kukamilisha kuitwa mama” ameandika Nandy

Aidha aliendelea kwa kuonesha furaha alionayo kwa kipindi hiki kwa kusema “nyie na furaha sijawahi kupata maishani mwangu nilijua nimefurahi na mengi lakini kumbe bado, hii ni furaha ya kweli toka moyoni mume wangu asante kwa zawadi hii asante kwa kunipa best friend na kumalizia kwa kusema new mom in town” ameandika Nandy

Aloooooh! Hongera nyingi kwao kwa Mr na Mrs Nenga kwa kuongeza familia tuseme tu mungu awabariki, usiache kudondosha komenti yako hapo chini ya kumtakia kheri mwanadada huyo.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post