Mastar waliodamshi kwenye harusi ya Nandy

Mastar waliodamshi kwenye harusi ya Nandy

Ikumbukwe kuwa tarehe 16 July, 2022 ilifungwa ndoa ya wasanii wa wakubwa hapa nchini Billnass pamoja mkewe halali kabisa, Nandy na kufanikiwa kuifanya sherehe yao katika ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es salaam.

Ebwana kama kawaida wiki hii inayomalizika bwana tulianza vizuri kabisa katika anga ya fashion nimekuandalia kali za mjini hususani kwa mastaa ambao walidamshi kuliko wengine, watoto wa mjini wanasema hivyo.
 

Mastaa mbalimbali na watu mashuhuri waliweza kujitokeza kwenye hafla hiyo ikiwemo Rais wa klabu ya Yanga Hersi Ali, viongozi kutoka Serikalini akiwemo Katibu Halmashauri kuu ya  CCM Taifa itikadi na Uenezi,  Shaka Hamdu Shaka bila kuwasahau wasanii wa bongo fleva na bongo movie pia.


Bila shaka hafla hiyo ilipambwa zaidi na kufurika kwa wasanii akiwemo Whozu, Alikiba, Wema Sepetu, Irene Uwoya, Steve Nyerere, Zamaradi Mketema, Shilole, Aunt Ezekiel, Dr. Cheni, Gigy Money, Millard Ayo, Meena Ally, Idris Sultan, Baba Levo, Mwijaku, Linah, Vunja bei na wengine kibao.

Ukiachana na hiyo sasa kubwa kuliko kwenye fashion tumekusogezea mastaa ambao walidamshi yaani walitokelezea katika shughuli hiyo bila shaka unawaona hapo kwa picha.

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Saphinia Suleiman

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, career, skills development and technology.


Latest Post