Mahakama yaamuru mwanafunzi aliyefukuzwa kurudishwa chuoni

Mahakama yaamuru mwanafunzi aliyefukuzwa kurudishwa chuoni

Baada ya kufukuzwa chuo kwa kosa la kufanyiwa mtihani na mwenzake, mwanafunzi washada ya kwanza ya sheria katika chuo cha Tumain Dar es salaam (TUDARCO) aliyefahamika kwa jina la Mwajuma Malulu.

Mahakama kuu imeamuru mwanafunzi huyo kurejeshwa chuoni na kuruhusiwa kufanya mitihani ya muhula wa 2.

Julai 21, 2022, Malulu aliandikiwa barua na chuo, akitakiwa kujieleza, ambapo alikanusha kumruhusu Bahati Mfaume kumfanyia mtihani wowote.

Mfaume alidai kuwa alimfanyia Malulu mtihani huo kwa kumuonea huruma kwa kuwa alikuwa nje ya chuo, akimhudumia mtoto wake mchanga.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post