Jinsi ya kupika cookies kwenye jiko la mkaa

Jinsi ya kupika cookies kwenye jiko la mkaa

Naam! Uko pouwa mdau wangu? hivi unafahamu namna ya kupika cookies? Au ndo unasikia sikia tu halafu helewi mambo, usijali hili suala niachie mimi.

Leo kwenye nipe dili nitakujuza namna ya kupika cookies yani biscuit tena kwakutumia jiko la mkaa tuingie jikoni mtu wangu.

Mahitaji

Mafuta ya Butter au Blue Band kiasi ya robo kg

Sukari ile laini robo

Unga wa ngano robo (All Purpose flour)

Namna ya kuandaa na kuoka biskuti

Kwanza changanya butter/blueband na sukari – vichanganye hadi vilaini kabisaaa, kisha ongeza unga wa baking hapo pia changanya sana vya kutosha hadi unga uwe washikana – kumbuka mahitaji ni hayo matatu usiongeze maji.

Baada ya kuwa umeuchanganya vema unga wako uhifadhi kwa friji au mahali tulivu kwa dakika 20 hivi.

Kisha Pasha jiko lako moto kama watumia oven au kama ni mkaa uwe tayari.

Baada ya hapo toa na ukande upya kisha tengeneza katika shape za biskuti unazozipenda.

 

 

 

Weka katika baking sheet kwa wanaotumia oven – weka katika oven biskuti zako – usiwe mbali na jiko kwani ndani ya dakika 15 – 20 zinatakuwa tayari pale utakapoona zinaanza kuwa brown katika kona na biskuti.

Zikiwa tayari wazitoa na kuacha zipoe kwa dakika 5 basi hapo zipo tayari.

Hapa sasa kwa wale watakaotumia jiko la mkaa fuata maelekezo haya.

Uwe na sufuria kubwa alafu punguza mkaa kabisa katika jiko ikiwezekana acha kijikaa kimoja kidogo sawa weka kisufuria kidogo ndani ya sufuria kubwa tafuta mfuniko wa bati – panga biskuti zako katika mfuniko wa ndani funika na mfuniko mkubwa weka jikoni kisha palililia mkaa mwingine kwa juu

Uwe unafunua kuchungulia kila baada ya dakika 5.

Yees! Mimi nimemaliza hivyo kazi kwako kwenye utendaji unaweza kutengeneza cookies na ukauza madukani ukajiingizia kipato kila la heri mtu wangu haina kufeli.

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Saphinia Suleiman

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, career, skills development and technology.


Latest Post