Drake afanyiwa vurugu jukwaani

Drake afanyiwa vurugu jukwaani

Msanii kutoka nchini Marekani Drake alishambuliwa jukwaani wakati akiperform wimbo wa ‘So Anxious’ kwa kurushiwa viatu, simu na nguo kutoka kwa mashabiki, katika usiku wa ufunguzi wa ziara yake ya ‘It’s All a Blur’ huko Chicago.

Matukio kama hayo yameonekana kuwa mengi nchini humo ambapo yanatajwa kuhatarisha usalama wa wasanii kwa kurushiwa vitu jukwaani wakati wakitoa burudani.

Hivi karibuni mwimbaji wa pop Bebe Rexha alilazwa hospitalini baada ya shabiki kumrushia simu  na kumgonga usoni kisha kusababisha jeraha la jicho. Wasanii wengine ni Adele, P!nk nao pia walikutana na kisanga kama hiki






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post