Diamond Platnumz athibitisha kudate na Zuu

Diamond Platnumz athibitisha kudate na Zuu

Huenda msanii wa Bongo Fleva nchini Tanzania, Diamond Platnumz akawa amethibithisha kuwa katika lindi la penzi zito na msanii mwenzake, Zuchu baada ya kutoa comment katika Post ya account ya Instagram ya wasafi wcb akiandika, "that's Zuu's husband."surprisedsurprisedlaughing

Mashabiki wengi wameinterpret hilo jina la "Zuu" kama kifupi cha "Zuchu."


Wawili hao wamekuwa wakihisiwa kuwa penzini mara baada ya kuvuja kwa video wakiwa katika gari ya Diamond na toka hapo wamekuwa wakifanya challenges na kutoa wimbo pamoja, ikiwemo 'Mtasubiri' kutoka kwenye EP ya FOA kutoka kwa Diamond.



Hata hivyo, 'Couple' hii imekuwa haiishiwi vituko vya kuzidi kuaminisha mashabiki wao kuwa wapo pamoja. Ukaribu wa kupindukia kati yao umeonekeana kukua kwa kiasi kikubwa, hadi kuonesha viashiria wazi wazi wakiwa stejini, mmmhhhh, nisiseme sana!sealedsealed



Kama wawili hao watakuwa ni wapenzi kweli, basi Zuchu atakuwa mwanamke sio chini ya wa 9 kutoka na msanii huyo mwenye watoto wa 4 kutoka kwa wanawake wa 3 tofauti, kutoka nchi 3 tofauti. Mambo hayolaughing



Hakuna kati yao aliyeconfirm moja kwa moja kuwa wanadate, ingawa Zuchu ameweka hadharani kuwa anadate na mtu na wanapendana sana.,,, aaawwwwwwink

Comment hiyo imewavuruga sana mashabiki. Tuambie, je unafikiri wawili hao wapo pamoja au la??






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Detricia Pamba

A Digital Journalist, Content Creation Executive at Mwananchi Communications Ltd and Chief Editor of Mwananchi Scoop. I'm also writes stories around Technology, every Wednesday on Mwananchi Scoop. My other famous segments on Mwananchi Scoop include LISTI and WHO’S HOT.


Latest Post