Diamond na Zuchu washinda tuzo za TDA

Diamond na Zuchu washinda tuzo za TDA

Usiku wa kuamkia leo msanii Zuchu na Bosi wake Diamond wameshinda tuzo za Tanzania Digital Awards(TDA) ambapo Diamond ameondoka na tuzo ya msani bora wa kiume wa mwaka anayetumia Digital kwa ufanisi (Digital Artist Of The Year Male) huku zuchu akiondoka na tuzo Digital Artist Of The Year Female.

Tuzo hizo za TDA zinalenga kukuza uwajibikaji, ubunifu na uvumbuzi katika matumizi ya teknolojia za kidijitali Tanzania katika sekta mbalimbali.

Kwa sasa Zuchu na Diamond wanakimbiza katika mitandao ya kijamii kufuatia na ngoma zao walizoziachi hivi karibuni ambapo Simba akitamba na kibao cha ‘Komasava’, Zuchu akiendelea kuwateka zaidi na wimbo wake mpya wa ‘Siji’.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post