Biden: Tunasimama na Ukraine

Biden: Tunasimama na Ukraine

Rais wa Marekani Joe Biden amesema nchi yake itasimama na Ukraine hadi mwisho wa mzozo wake dhidi ya Urusi.

Biden amemuambia Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky kuwa hatasimama pekee yake katika vita hivyo na atambue kuwa Marekani ipo nyuma yake.

Ameyasema hayo Zelensky alipotembelea Ikulu ya White House ikiwa ni ziara yake ya kwanza nje ya nchi tangu uvamizi wa Urusi uanze.

Aidha Rais Zelensky ameishukuru Marekani kwa msaada inayoendelea kuutoa huku akiahidi kuwa utawala wake hautajisalimisha mbele ya Urusi hata siku moja na watapambana hadi mwisho.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post