Ayra kwenye ziara ya Chris Brown

Ayra kwenye ziara ya Chris Brown

Mwanamuziki kutoka nchini Nigeria, Ayra Starr amepewa shavu na mwanamuziki Chris Brown kuwepo kwenye ziara yake iliyopewa jina la ‘11:11’ ambayo imebeba jina la album ya Brown.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Breezy ame-share taarifa hiyo ambapo mwadada Ayra Starr atakuwa kwenye ziara ya Breezy katika miji 26 ikiwemo Canada, Marekani, Washington DC, Toronto na mingineyo.

Ziara hiyo inatarajiwa kuanzia mjini Detroit Juni 5 na kumalizika Los Angeles, Agosti 6 mwaka huu 2024, Chris Brown anamualika Ayra Starr kama mgeni maalum ‘Special Guest’ katika tour hiyo, huku samnii mwingine akiwa ni Muh Knee Long.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post