Wiz Khalifa ataka heshima

Wiz Khalifa ataka heshima

Star wa Hip Hop kutokea nchini Marekani, Wiz Khalifa amewaonya mastaa wenzake kuwa wanatakiwa kuishi vizuri na kuheshimiana hasa kuelekea kipindi cha mwaka mpya.

Msanii huyo ametupia ujumbe huo katika ukurasa wake wa Twitter ambapo amesema katika kuwaenzi marapa wenzao Drakeo Theruler na Young Dolph anawaomba wasanii wenzake kuishi kwa Amani.

“As enternainers lets try some shit next year. Minding our own business, not dis respecting each others family, dead homies or area they come from. Stop using someone else’s significant other as a one up to the other person, Actually showing the same love you expect to get,” ameandika akimaanisha

“Kama waburudishaji tujaribu kitu kipya mwaka ujao, tujali mambo yetu binafsi, tusidharauliane familia zetu, wafu au mahali mtu anakotoka. Tusichukulie madhaifu ya mtu kumweka chini na kumjia juu. Tuoneshe upendo ambao wewe binafsi unatarajia kupata kutoka kwa wengine,”

 

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm


Latest Post