Will Smith alia na wasioangalia filamu yake mpya

Will Smith alia na wasioangalia filamu yake mpya

Muigizaji maarufu nchini Marekani Will Smith awajia juu waliobeza ujio wake kwenye filamu yake mpya alioipa jina la Emancipation inayotajwa kutofanya vizuri na hiyo inasemekana ni kutokanana na  kufuatia kitendo chake cha kumzaba kofi msanii mwenzake na mchezashaji Chris Rock.

ikumbukwe tuu Will alimchapa kofi baada ya Chris kufanyia mzaha muonekano wa mke wake Jada Pinkett Smith, ambapo kwa mujibu wake wakati wa utetezi alisema muoneko huo ni kwa sababu ya maradhi yanayomsumbua mke wake.

Smith hakulikalia kimya jambo na kuamua kusema anaelewa watu kutoitizama filamu yake kufuatia kitendo hicho, na kwamba wana kila sababu ya kumuadhibu kwa kuwa anawaelewa.

Filamu yake hiyo, inahusu harakati za Peter (Will Smith), ambaye ni mtumwa, aliyekimbia shamba huko Louisiana baada ya kuchapika kimaisha.

Haya wabongo wenzangu najua tunaelewa sana move sa huyu mwamba embu tumfute machozi kwa kuenda kuangalia kigongo chake, yaani kama kawada yake sio pouwa.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post