Wakili agoma kutumia lugha ya Kingereza mahakamani

Wakili agoma kutumia lugha ya Kingereza mahakamani

Wakati lugha ya Kiswahili ikizidi kuvuka boda na kuleta mafanikio mazuri katika nchi mbalimbali kuweza kuruhusu lugha hiyo itumike kimataifa kama lugha ya Kingereza, huko nchini Kenya wakili mmoja aliejulikana kwa jina Harrison Kinyanjui.

Alikataa mbele ya mahakama kuu jijini Nairobi kuongea na Jaji Lawrence Mugambi pamoja na mawakili wengine kwa kutumia lugha ya Kingereza.

Kwa kutoa ombi mbele ya mahakama kutumia lugha ya Kiswahili akidai kuwa ni lugha ya taifa ndipo Jaji mkuu alipo chukua jukumu la kughairisha kesi hiyo.

Mpaka atakapo patikana mkalimani baada ya wakili huyo kukataa matumizi ya lugha ya kingereza katika hukumu ya kesi.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post