Vituo 24 vyafungiwa baada ya kufanya udanganyifu

Vituo 24 vyafungiwa baada ya kufanya udanganyifu

Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) limevifungia vituo vya kufanyia mitihani 24 sawa na asilimia 0.13 ya vituo vyote 17,935 vilivyofanya mtihani ambavyo vimethibitika kupanga na kufanya udanganyifu katika mtihani wa kumaliza elimu ya msingi (dalasa la saba) 2022.

Vituo hivyo vimefungiwa hadi Baraza litakapojiridhisha kuwa ni salama kwa uendeshwaji wa mitihani, vituo hivi ni Kadama Primary (Chato), Rweikiza Primary (Bukoba), Kilimanjaro Primary (Arusha), Sahare Primary (Tanga), St.Anne Marie Primary (Ubungo, Dar es salaam) ,

Vituo vingine vilivyofungiwa ni Ukerewe Primary (Mwanza), Peaceland (Ukerewe), Karume Primary (Bukoba) , Al Hikma Primary (Dar es salaam) Kazoba Primary (Karagwe), Mugini Primary (Magu Mwanza), Busara (Magu, Mwanza), Jamia Primary (Bukoba) Winners Primary (Mwanza), Musabe Primary (Mwanza ),

Aidha vituo vingine vilivyofungiwa ni Elisabene Primary (Tunduma), High Challenge Primary (Arusha), Tumaini Primary (Sengerema Mwanza), Holele Primary (Mwanza) Must Lead Primary (Chalinze) Moregas Primary (Tarime) Leaders Primary (Rorya), Kivulini Primary ( Mwanza) , St Severin Primary (Biharamulo).






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post