Unalifahamu tundu dogo la kufuli, Hii hapa kazi yake

Unalifahamu tundu dogo la kufuli, Hii hapa kazi yake

Miaka ya nyuma watu wengi walikuwa wakitumia makomeo ya kufunga na kufuli kwa ajili ya kulinda usalama wa mali zao za ndani, ingawa wapo wanaotumia hadi sasa lakini wengine wameenda mbali zaidi, huzitumia kufunga kwenye masanduku ya bati ya kuhifadhia vitu mashuleni.

Licha ya kuwepo kwa makampuni mengi ya kutengeneza kufuli, lakini yote huzitengeneza zikiwa na tundu dogo pembeni ya tundu la kuingizia funguo, wapo baadhi ya watu ambao wamekuwa wakiliona tundu hilo bila ya kufahamu sababu ya kuwekwa kwenye kufuli. hivyo basi fahamu kuwa tundu limewekwa kwa kazi yake maalumu.

Kutokana na mazingira ambayo kufuli hutumiwa kufunga nyumba wakati mwingine hupelekea kupata unyevu au kunyeshawa na mvua maji huingia ndani ya kufuli, hivyo basi tundu hilo dogo pembezoni mwa tundu la kuingiza funguo limewekwa kusaidia kutoa nje maji yatakayoingia kwenye kufuli.

Hata hivyo kutokana na maji au unyevu ndani ya kufuli hulipelekea kupata kutu na kusababisha ugumu kwenye kufunguka. Kwa hiyo kwa kutumia tundu hilo dogo mtumiaji anaweza kulitumia kuweka mafuta kwa ajili ya kulainisha sehemu za ndani za kufuli ambazo hazionekani na kuondoa au kuzuia kutu ndani yake
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post