Saudia hawana ubahili kwenye soka

Saudia hawana ubahili kwenye soka

Muanzilishi wa kampuni ya ‘FutBolJobs’ Valentin Botella Nicolas, kutoka nchini Saudi Arabia amepanga kusajili wachezaji wapya kwa ajili ya ‘ligi’ daraja la tatu ambao watalipwa tsh 8.2 milioni hadi tsh 10.9 milioni kwa mwezi pamoja na kupewa makazi ya kuishi.

Inaelezwa kuwa Valentin ndio msimamizi mkuu wa mchakato huo huku akiwataka wachezaji wenye nia kukimbilia furusa hiyo ya kucheza ‘ligi’ daraja la tatu.

Huku ikiwekwa wazi kuwa uwepo wa nyota wakubwa wa ‘Soka’ nchini humo kama Cristiano Ronaldo, Sadio Mane, Neymar Jr, Karim Benzema na wengineo kumeongeza umaarufu wa ‘ligi’ hiyo.

Hata hivyo Saudia ndio nchi ambayo inamwaga mpunga mrefu kwa wachezaji wake akiwemo #CristianoRonaldo kulipwa tsh 564 bilioni, KarimBenzema tsh 318 bilioni na SadioMane tsh 109 bilioni.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post