Sadaka zaibiwa madhabahuni

Sadaka zaibiwa madhabahuni

Paroko wa Parokia ya Narumu, Kata ya Machame, mkoani Kilimanjaro, Padri Thomas Chuwa, amedai kuwa kapu lililokuwa na sadaka za misa limeibiwa katika mazingira ya kutatanisha.

Amesema sadaka zilizoibiwa zilikuwa ni matoleo ya shukrani, vipaji na sadaka ya misa takatifu katika ibada ya misa ya kwanza.

Padre huyo amewaasa waumini wa Kanisa hilo kusali sala maalum kwa muda wa siku 3 kwa ajili ya watu/mtu aliyeiba, ambapo amesema kitendo hicho ni kibaya kwa Kanisa lakini anamkabidhi Mungu.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post