Saa za Apple zinazopima Oxygen zazuiwa Marekani

Saa za Apple zinazopima Oxygen zazuiwa Marekani

Kampuni ya simu Apple ambayo pia inatengeneza saa imezuiliwa kuuza ‘Apple Watch’ ambazo zimetengenezwa kwa mfumo unaopima kiasi cha Oxygen kwenye damu nchini Marekani.

Saa hizo aina ya Series 9 na Ultra 2 zimezuiliwa kuuzwa kutokana na madai ya kuiba mfumo huo kutoka kwa kampuni ya #Masimo, kufuatiwa na tuhuma hizo Apple imeshindwa kesi hiyo iliyosikilizwa siku ya jana Alhamis katika Mahakama ya Rufaa ya Marekani kutokana na kuiba haki miliki ya #Masimo.

Hivyo basi ili Apple iweze kuuza saa zake nchini Marekani inatakiwa kuzima mfumo huo kuanzia siku ya jana.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post