Rick Ross yupo mbioni kujenga nyumba chini ya ardhi

Rick Ross yupo mbioni kujenga nyumba chini ya ardhi

‘Rapa’ kutoka nchini Marekani Rick Ross ameweka wazi kuwa anampango wa kujenga nyumba chini ya Ardhi ambayo itakuwa na chumba cha kulala, gereji na mashine inayotengeneza maji kutoka angani.

Kupitia video inayosambaa mitandaoni inamuonesha Rick akieleza kuwa atajenga chumba hicho kwa lengo la kujiandaa na maisha yake ya siku ya mwisho.

Mbali na kutaka kujenga mjengo huo Rick pia anamiliki ndege binafsi (private jet), eneo la hekari 2.3 kwa ajili ya mapumziko lililopo Florida, na Jumba la kifahari la ‘Star Island Waterfront'.

Ikumbukwe pia baadhi ya matajiri dunia kama vile Elon Musk na Mark Zuckerberg tayari wamejenga nyumba za aina hiyo chini ya ardhi,zijulikanazo kama ‘Bunkers’.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post