Rick Ross akabidhiwa funguo ya jiji la Miami

Rick Ross akabidhiwa funguo ya jiji la Miami

Meya wa jiji la Miami Francis Suarez na Mbunge Frederica Wilson kutoka nchini Marekani siku ya Jana, Januari 15 wamemkabidhi ‘Rapa’ Rick Ross ufunguo wa jiji la Miami, huku akitangazwa kuwa muziki wake utaingia katika maktaba ya Congress.

Ross siyo msanii pekee ambaye ametunukiwa ufunguo wa heshima katika mji aliotokea, ikumbukwe kuwa wapo ma-staa ambao pia wamewahi kutunukiwa heshima hiyo akiwemo ‘rapa’ Drake, Wiz Khalifa na mwengineo.

Maktaba ya Congress ndiyo maktaba kubwa zaidi duniani, ikiwa na mamilioni ya vitabu, filamu na video, nyimbo, picha, magazeti na ramani. Maktaba hiyo inatumika kama chombo kikuu cha utafiti cha Bunge la Marekani na makao ya Ofisi ya hakimiliki ya U.S.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post