Papa Francis kukutana na viongozi wakuu wa kiislamu leo

Papa Francis kukutana na viongozi wakuu wa kiislamu leo

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis anatazamiwa kukutana leo na viongozi wakuu wa dini ya Kiislamu, akiwa katika ziara nchini Bahrain inayoazimia kuboresha mjadala baina ya imani tafauti.

Papa Francis aliwasili jana katika taifa hilo la Ghuba ya Arabuni, akatoa hotuba iliyokosoa adhabu ya kifo na kuhimiza mataifa kuheshimu haki za binaadamu na kuweka mazingira bora kwa wafanyakazi.

Makundi ya kutetea haki za binaadamu yalikuwa yamemrai Papa kuangazia madai ya unyanyasaji unaofanywa na ufalme wa Bahrain unaoongozwa na wafuasi wa madhehebu ya Sunni katika taifa hilo ambalo raia wengi ni wa madhehebu ya Shia.

Leo Ijumaa Papa Francis anakutana na Sheikh Ahmed al-Tayeb, Imam mkuu wa msikiti wa Al-Azhar wa mjini Cairo, Misri, ambao ni kituo kikuu cha mafunzo ya madhehebu ya Sunni.

Papa Francis ameufanya mjadala baina ya dini tofauti kuwa kiini cha uongozi wake, na amezizuru nchi kadhaa za Kiislamu zikiwemo Uturuki, Misri na Irak.

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Saphinia Suleiman

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, career, skills development and technology.


Latest Post