Mwandishi wa habari aliegoma kula kwa siku kadhaa  apelekwa hospital baada ya afya kuzorota

Mwandishi wa habari aliegoma kula kwa siku kadhaa apelekwa hospital baada ya afya kuzorota

Mwandishi wa habari maarufu na mkosoaji wa serikali ya Senegal ambaye amekuwa kwenye mgomo wa kula kupinga mashtaka dhidi yake amehamishiwa hospitalini baada ya afya yake kuzorota.

Wakili wa Pape Ale Niang ambae ni mkuu wa tovuti ya habari ya mtandaoni ya Dakar Matin, amesema aligoma kula mnamo Desemba 2 baada ya kuwa kizuizini kwa wiki kadhaa na baadae alilazwa hospitali na kuachiliwa kwa muda kabla ya kukamatwa tena Decemba 20.

Aidha mwandishi huyo alikamatwa Novemba 6 na kushtakiwa kwa kufichua habari zinazoweza kuhatarisha usalama wa taifa.Kesi dhidi yake iliibuka baada ya kuandika kuhusu mashtaka ya ubakaji yanayomkabili kiongozi mkuu wa upinzani nchini humo, Ousmane Sonko.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post