Mudathir na Feitoto kukosa ‘mechi’ tatu

Mudathir na Feitoto kukosa ‘mechi’ tatu

‘Mastaa’ wawili wa ‘klabu’ ya #Yanga na Azam FC inadaiwa kuwa wanatarajia kuingia kwenye faini TSh 500,000 na kufungiwa ‘mechi’ tatu kutoka bodi ya ‘ligi’ kutokana na kitendo walichokifanya kwenye mchezo wa juzi, Jumatatu.

Baada ya Feisal Salum na Mudathir Yahya kuzua taharuki kwa kutegeana kuingia eneo la kuchezea la Uwanja wa Benjamin Mkapa. Tukio hilo lilitokea wakati vikosi vya ‘timu’ hizo vikiingia uwanjani hapo tayari kuanza dakika 45 za kipindi cha kwanza na wachezaji hao walisimama kwenye mstari wa kuingia eneo la kuchezea.

Kwa mujibu wa kanuni ya 41:5 (5.4), kufanya kitendo chochote cha aibu, kama vile kukojoa uwanjani, kukataa kupeana mkono na mgeni rasmi, waamuzi na wachezaji wa timu pinzani, kutoa au kuonyesha ishara inayoashiria matusi ni kosa.

Fei Toto alikuwa anafanya mazoezi ya viungo kwa kunyoosha miguu huku Mudathir akikung’uta viatu vyake ili kuvuta muda wa nani awahi kuingia uwanjani kitendo ambacho bodi ya ligi inatafsiri kama imani za kishirikiana na kutoza faini.

Ikumbukwe kuwa msimu uliopita mastaa wa Simba na Yanga Aziz KI na Clatous Chama, walilipishwa faini ya Sh500,000 na kufungiwa kutokucheza ‘mechi’ tatu za ‘Ligi’ Kuu zilizokuwa zinafuata kwa kosa kama hilo.

 Credit @mwanaspoti
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post