Mo Music: Baba Levo alistahili

Mo Music: Baba Levo alistahili

Mwanamuziki wa #BongoFleva, #MoMusic ameeleza kuwa #BabaLevo alistahili kupigwa na #Harmonize, huku akidai kuwa hata angekuwa yeye angefanya hivyo hivyo.

Mo ameyasema hayo kupitia mahojiano na moja ya chombo cha habari nchini kwa kueeleza kuwa inauma sana mtu anapokusema vibaya katika utafutaji wako bila kujali changamoto unazopitia, ambapo alidai kuwa Harmonize alikuwa sahihi kumpiga #BabaLevo.

Ikumbukwe kuwa week iliyopita Baba Levo ‘aliposti’ katika ukurasa wake wa Instagram akidai ameshambuliwa na Harmonize bila kueleza sababu ya shambulio hilo na amedai kuwa kwasasa kesi hiyo iko polisi.

Huku kwa upande wa mwanamuziki Harmonize hajazungumza chochote mpaka sasa.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post