Miwani zenye saini ya Diddy zasitishwa kuuzwa

Miwani zenye saini ya Diddy zasitishwa kuuzwa

Kampuni ya America's Best Contacts & Eyeglasses imeripotiwa kusitisha kuuza fremu za miwani zenye saini ya Diddy kutokana na kuhusishwa kwenye kesi kadhaa za unyanyasaji wa ngono.

Kwa mujibu wa Tmz taarifa hiyo imethibitishwa na mwakilishi wa kampuni hiyo kwamba maduka hayo yalianza kuacha kuuza fremu zenye saini ya Diddy Jumanne iliyopita huku zikiuzwa za kawaida ambapo mpaka sasa haijawekwa wazi kuwa fremu hiza za Combs zitapelekwa wapi.

Ingawa kampuni hiyo haikufichua sababu kamili ya hatua hiyo, lakini kilingana na wadau mbalimbali wamedai kuwa uamuzi huo unahusishwa wazi na hisia za umma kufuatia na video iliyosambazwa wiki iliyopita ikimuonesha Diddy akimpiga aliyekuwa mpenzi wake Cassie.

Mpaka kufiki sasa Diddy amehusishwa kwenye kesi saba za unyanyasaji wa kingono huku ya mwisho ikifunguliwa siku tatu zilizopita na aliyekuwa mwanafunzi wa Taasisi ya Teknolojia ya Mitindo aitwaye Lampos.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post