Meja Kunta: Watanzania naombeni dua zenu

Meja Kunta: Watanzania naombeni dua zenu

Wakati wasanii wa #BongoFleva wakiendelea kukiwasha katika sekta yao huku watoto wa uswazi wazee wa singeli wakiendelea kupambana ili kuufikishe muziki wa singeli kimataifa.

Muimbaji wa singeli nchini Mejakunta kupitia #InstaStory yake ameweka ujumbe akieleza kuwa anaomba baraka za watanzania kwa ajili ya kuupeleka muziki huo kimataifa .

Katika kuomba apewe baraka lakini pia Meja amedai kuwa muziki huo utabadilisha mawazo ya watu wengi kwani singeli inaenda kimataifa. Meja ameandika,

“Now singeli inatoboa international na hii itakuja kubadilisha mawazo ya watu wengi sana, sababu wanyamwezi watazicheza sana (singeli ndio mziki wa kinyamwezi) soon nitailisha dunia chakula bora, kula chuma hicho

Sasa nimebakiza project za international tu hivyo naomba baraka za watanzania wenzangu na support kwa wasanii wote #safarindioinaanza naombeni dua zenu #timetoadvertise”






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post