Mambo 13 usiyoyajua kuhusu Kakakuona

Mambo 13 usiyoyajua kuhusu Kakakuona

Msomaji wetu tunatumaini kuwa u mzima wa afya na unaendelea vema na majukumu yako ya kila siku.

Basi leo katika kipengele cha listi tumekusogezea mambo 13 usiyoyajua kuhusu kakakuona, najua wengi wetu jina la mnyama huyo tumeshawahi kulisikia basi ungana nasi kuelewa na kufahamu mengi zaidi.

Inakadiriwa kuwa mnyama huyo huishi kwa kipindi cha miaka 20 akiwa katika pori. Lakini hiyo ilikuwa inafahamika zamani kipindi ambacho mnyama huyo alikuwa anaonekana tofauti na sasa.

Moja ya mambo hayo ni kuwa kuna aina nane za kakakuona

Inaelezwa kuwa kuna aina hi nane za kakakuona zimetoka katika familia inayofahamika kama manidae. Aina hizo za kakakuona zipo duniani kwa zaidi ya miaka 80 milioni ya mabadiliko yao.

Kati ya hizo, aina nne za kakakuona zinapatikana katika Bara la Ulaya na wengine barani Afrika. Hawa wanafahamika kwa majina ya tree kakauona, giant kakakuona, cape kakakuona na kakakuona wenye mkia mrefu.

Mbili, Ana ulimi mrefu kuliko mwili wake

Kakakuona ana ulimi wenye urefu unaozidi mwili wake.

Akiurefusha kwa kuutoa nje ya kinywa unafikia urefu wa sentimita 40.

Ulimi huo ambao pia unanata, huutumia kwa ajili ya kukusanya wadudu ambao ndiyo mlo wake wa pekee, hana mwingine zaidi ya huo kutokana na kukosa meno.

Tatu, Ndiye mnyama pekee duniani ambaye mwili wake umefunikwa na magamba makubwa

Magamba yanayofunika mwili wa mnyama huyo ni makubwa kuliko ya viumbe wengine. Magamba hayo kitaalamu yameundwa na kitu ninachoitwa ‘keratin’, ambayo yanafanana na yale yanayounda kucha za binadamu.

Asilimia 20 ya uzito wa mwili wa mnyama huyo unatokana na magamba.

Kakakuona hutumia magamba hayo kama silaha ya kujilinda dhidi ya maadui.

Nne, Maana ya jina "kakakuona"

Maana ya jina hilo ilianzia nchini Malaysia, Indonesia na Brunei likimaanisha "kitu kinachojikunja". Kakakuona hupenda kujikunja kama mpira.

Hiyo ikiwa kama mbinu anayotumia kujilinda dhidi ya maadui.

Licha ya kuwa hutumia mbinu hiyo kujilinda, lakini anapojikunja ndiyo inakuwa rahisi kwa watu kumkamata na kumbeba.

 

 

Tano, huishi juu ya miti na kwenye mashimo.

Baadhi ya kakakuona huishi juu ya miti, wengine hujichimbia ardhini na kuishi ndani ya mashimo.

Wengi wanaoishi juu ya miti ni wale wenye mikia mirefu wanaopatikana barani Afrika.

Wengine huchimba mashimo marefu ardhini na kuishi humo ili wasikutane na binadamu.

Sita, Ni mwepesi kushambuliwa na wanyama wengine.

Ukiachilia mbali adui yao mkubwa ambaye ni binadamu, adui wengine wa wanyama huyo ni jamii ya chui na simba.

Hata hivyo, maadui hao hushindwa kuwashambulia kakakuona kutokana na namna wanavyojilinda kwa kujikunja na jinsi mwili wao ulivyo na magamba. Kutokana na hali, hiyo inakuwa vigumu kwa simba au wanyama wengine kuwashambulia kwa kuwala.     

Saba, Hakuna anayefahamu miaka anayoishi.

Inakadiriwa kuwa mnyama huyo huishi kwa kipindi cha miaka 20 akiwa katika pori.

Lakini hiyo ilikuwa inafahamika zamani kipindi ambacho mnyama huyo alikuwa anaonekana tofauti na sasa.

Hata hivyo, kutokana na aina ya maisha ya wanayoishi, inasemekana kuwa wanaweza wasiishi miaka mingi, licha ya kuwa bado haifahamiki kwa sasa, inawezekana wakaishi kwa miaka 20.

Nane, Hutema sumu kali kama timdikali

Kakakuona akiona adui hujilinda kwa kujikunja, lakini akiona hali inakuwa mbaya zaidi, hutema sumu kali mithili ya tindikali inayoweza kumdhuru adui.

Pia, wakati mwingine hunyoosha mkia wake na kuuzungisha na kumkata adui aliyekaribu yake.

Tisa, Mamilioni wameuawa na kuuzwa ndani ya miaka 10.

Inakadiriwa kuwa kakakuona 100,000 hukamatwa kila mwaka barani Afrika na Ulaya na kuuzwa.

China na Vietnam ndizo nchi maarufu ambazo nyama na magamba yake huuzwa.

Kutokana na hilo, Shirika la Umoja wa Mataifa la Hifadhi za Asili (IUCN) limemweka kakakuona kwenye orodha ya wanyama walioko kwenye hatari ya kutoweka duniani.

10, Hawaoni vizuri

Ni aina moja katika ya nane za kakakuona wenye uwezo wa kuona vizuri hasa muda wa mchana.

Hawa ni wale wanaopatikana barani Afrika.

Wengine hawana uwezo wa kuona vizuri kutokana na kuwa na macho madogo.

11, Wana uwezo mkubwa wa kunusa na kusikia

Licha ya wengine kuwa na macho madogo na kushindwa kuona vizuri, kakakuona ni mnyama mwenye uwezo mkubwa wa kusikia sauti yoyote kwa haraka kwa sababu masikio yake yameinuka. Pia, ana uwezo mkubwa wa kunusa harufu yoyote.

12, Ni vigumu kujamiiana

Tofauti ilivyo kwa baadhi ya wanyama, upande wa kakakuona tendo kujamiiana ni gumu kutokana na tofauti za kimwili kati ya jike na dume. Mwili wa kakakuona dume una uzito mkubwa zaidi ya asilimia 50 ukilinganishwa na jike.

Mbali na hivyo, hawana msimu maalumu kukutana na kujamiiana, tofauti na ilivyo kwa wanyama wengine kama binadamu.

13, Uhusiano na wanyama wengine.

Imezoeleka kuwa, mnyama huyo huwa karibu na wanyama wengine wa jamii yao, kwa maana ya wale wanaokula wadudu.

Hata hivyo, hivi karibuni wanasayansi wamebainisha kuwa wamekuwa karibu na wanyama kutoka jamii nyingine kama wale wanaokula nyama






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm


Latest Post