Mabondia wapata fursa kuweka kambi Cuba

Mabondia wapata fursa kuweka kambi Cuba

Tanzania kupitia Wizara ya Utamaduni, Michezo na sanaa na Serikali ya Cuba wafanya makubaliano kushirikiana katika kuendeleza mchezo wa ngumi.

Ikiwemo  mabondia wa Tanzania watapata fursa ya kuweka kambi nchini Cuba, na walimu wa ngumi, pia mabondia kutoka Cuba watakuja Tanzania kufundisha na kubadilishana ujuzi.

Makubaliano hayo yamefanyika Agosti 2, na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ya Tanzania na Taasisi ya INDER ya Cuba.

Taasisi hiyo tayari ina mashirikiano na baadhi ya nchi za Afrika ikiwemo Algeria ambapo hubadilishana uzoefu kwenye eneo la mchezo wa ngumi.

Wakati Naibu Waziri, Mhe. Hamis Mwinjuma, (Mwana FA) alipokutana na Makamu wa Rais wa Taasisi ya Kitaifa ya Michezo, Elimu na Burudani nchini humo.

Credit @wizara_sanaatz






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post