Maambukizi ya VVU yaongezeka, Mara

Maambukizi ya VVU yaongezeka, Mara

Kiwango cha maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi mkoani Mara kimeongezeka kutoka asilimia 3.6 miaka mitano iliyopita hadi kufika asilimia 5 mwaka jana.

Hali hiyo inatokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kiuchumi na kijamii huku jamii ikitakiwa kushiriki moja kwa moja katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo.

Takwimu hizo zimetolewa leo, Desemba 12, 2023 na Mratibu wa Upimaji Ukimwi na Tohara Kinga Mkoa wa Mara, Felix Mtaki kwenye mafunzo ya waandishi wa habari yaliyoenda sambamba na utambulisho wa mradi wa Afya Thabiti.

“Hali ni mbaya kuna kila sababu ya kila mmoja kushiriki katika mapambano haya, kiwango hiki ni kikubwa kuliko hata kiwango cha Taifa ambacho ni asilimia 4.5,” amesema.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post