Lazima hiphop iwe na beef kama Bongo Fleva

Lazima hiphop iwe na beef kama Bongo Fleva

Baada ya kuwepo na ushindani katika muziki wa bongo fleva kumekuwa na maoni ya watu wengi kuwa ushindani huo uhamie katika #HipHop na mashabiki watoe ushirikiano kama wanavyoshabikia Bongo Fleva.

Kupitia tweet ya mtangazaji wa radio moja maarufu nchini, #Jabirsalehtherealest ameandika kuhusu wasanii wa hiphop kupewa ushirikiano pale wanapo raruana kwenye diss track, huku akitolea mfano wa mwanamuziki wa #HipHop #Rapcha_tz, kuwa ana kazi kubwa lakini kwa sababu sio diss track basi kuna ushirikiano anakosa.

#Jabirsalehtherealest kwenye ukurasa wake wa Twitter ameandika,

“Game ya #HipHop imechangamka, tunataka diss kama hizi, kauli hizi husikitisha sana, ku-suport rapa na wanahiphop ni mpaka wararuane na kuna wakati wanatoa ngoma kali, Rapcha ameachia mzigo mkali sana una mawe makali karibu yote, ila kwakuwa sio diss kama ile kwa D kimya”.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post