Jinsi ya kubalance masomo na kufanya mambo mengine chuoni

Jinsi ya kubalance masomo na kufanya mambo mengine chuoni

Hellow! I hope mko good kabisa watu wangu wa nguvu kama kawaida katika kipengele chetu cha unicorner tuko na mada hatari sana ambayo itakusaidia sana kubalance muda wa kujisomea na mambo yako mengine,

Ukiwa chuo hasa mwisho wa semester unaweza kushtushwa na vile muda ulivyokwenda haraka, mwanzo wa semester mnapofanya usajili mambo yanakuwa bado hayajachanganya.

Huu ndio muda wahadhiri wanapeleka vipindi mbele na wewe unalala sana. Kuna kipindi hapo katikati test, assignment na lectures zinachanganya na unakuwa busy kidogo yani mambo yanaanza kasi ya ajabu wabongo tunaita kasi ya 4G na kipindi cha mwisho ni pale unakaribia na unaingia UE/SE, yani hapa ndio kipindi unachoshangaa na kuwaza muda ulipotelea wapi.

Mara nyingi hii inatokea kwasababu ulikuwa unaenda tu kama mambo yalivyo haukuweza balance mambo yako, maana chuo kina mambo mengi yanaweza kukufanya hata ukashindwa kupata muda wa kujijali mwenyewe.

Haina shida, kama ungependa kujua jinsi ya kubalance mambo ya chuo na mambo yako mengine kama biashara nk, basi ungana nasi kujua nini ufanye ili kubalance time yako mtu wangu wa nguvu.

  • Pangilia ratiba zako Fanya mambo yako kwa wakati, kuwa na ratiba na schedule, maintain a consistent schedule (jitahidi kwenye swala la time management)

Kila swala lifanye katika muda uliopanga, kama ni masomo, soma kwa wakati uliopanga. Kama ni bata, kula vizuri tu kwenye wakati ulioupanga. Pumzika vizuri ili pia upate nguvu ya kufanya hivyo vitu unavyopanga kwa wakati.

  • Kama unabiashara Omba msaada

Kama una biashara room, ukienda lecture waombe ndugu, jaama wanaobakia wakuuzie Kama upo group la discussion na upo kwenye birthday party nyumbani au mbali, omba watu ulionao group moja wakusaidie kujua ni jinsi gani unavyoweza kushiriki hata ukiwa mbali au wakuandike jina kwenye assignment yenu hiyo ili usikose maksi. Usiogope kuomba msaada kama una mambo mengine na uko na watu waelewa.

  • Jitahidi kusoma kwa discussions, kusolve past papers na kuhudhuria lectures ili ukikaa kusoma usiwe unatumia muda mwingi sana kuelewa na kukalili.
  • Punguza kutumia muda kwenye vitu vinavyokuondolea focus unapofanya mambo unayoyafanya. Mfano kufanya challeng tiktok, hujakatazwa kufanya ila fanya kwa kujifurahisha tuu dakika chache basi. Pia epuka sana kushinda kwenye mitandao ya kijamii pasipo na jambo la msingi

Unaweza shangaa ni muda kiasi gani unaupoteza kuangalia umbea wa Instagram muda unaoanza kusoma au kusikiliza stori badala ya kwenda discussion au kwenye mishe zako nyingine.

Tafuta namna ya kubalance lakini jua katika lolote lile masomo yanakuja kwanza  Ukiwa kiongozi wewe ni mwanachuo mwenye cheo na dhamana yaa uongozi, ukiwa unafanya biashara jua pia wewe ni mwanachuo mwenye biashara, mambo yote yanakuja baada ya masomo kwahiyo jua pia wapi kwa kuweka uzito zaidi kwa wakati huo.

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post