Je wajua Mamba anauwezo wa kuzaa bila dume

Je wajua Mamba anauwezo wa kuzaa bila dume

Wana sayansi kutoka nchini Marekani, wamethibitisha kuwa mamba ni mmoja kati ya wanyama ambao wana uwezo wa kupata ujauzito na kuzaa bila ya mamba dume.

Kwa mujibu wa tovuti mbalimbali kutoka nchini Marekani zimeeleza kuwa wana sayansi hao waliligundua hili kwenye moja ya kambi ya wanyama huko Costa Rica.

Ambapo mamba mmoja aitwaye ‘Cocodrilo Parque Reptilandia’ mwaka 2018 alitaga mayai bila ya kupandwa na Mamba dume na kufanikiwa kutotoa mtoto mmoja.

Na hii ilikuwa ni mara ya kwanza kugundulika na kuingizwa kwenye tafiti kuwa Mamba ni mmoja kati ya wanyama ambao jike anaweza kutaga bila kupandwa, kitendo hicho kitaalamu huitwa parthenogenesis
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post