Jaji Warioba: tujibu hoja za dkt. Bashiru, kukosoa sio jambo baya

Jaji Warioba: tujibu hoja za dkt. Bashiru, kukosoa sio jambo baya

Kauli ya Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba, inafuatia majibu ya Watu mbalimbali Mtandaoni wanaodai Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM na Balozi, Dkt. Bashiru hana sifa za kuikosoa Serikali wakati hakufanya hivyo alipokuwa na Madaraka kwenye Utawala wa Hayati Rais Magufuli.

Warioba amesema Watu wamelikuza sana suala hilo wakati Dkt. Bashiru ana hoja ya msingi hasa kwa kuwataka Wakulima waungane na kuwa na sauti moja kuhusu mustakabali wao.

Dkt. Bashiru akizungumza na Wakulima hivi karibuni alitoa kauli zinazodaiwa kukosoa Serikali, jambo lililofanya akemewe vikali huku wengine wakimtaka ajiuzulu Ubunge.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Saphinia Suleiman

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, career, skills development and technology.


Latest Post