Israel yachukizwa na kauli ya Elon Musk

Israel yachukizwa na kauli ya Elon Musk

Taifa la Israel limekasirishwa na kauli ya mfanyabiashara Elon Musk kusaidia Gaza kurudisha mawasiliano, ni baada ya hivi karibuni mmliki huyo wa mtandao wa X kutoa ahadi ya kupeleka mawasiliano huko Gaza.

 Kwa mujibu wa vyombo vya habari inaelezwa kuwa bado Elon ameonekana kudhamiria kwa dhati kuisaidia Gaza kurudisha mawasiliano kama zamani ambapo kwasasa nchi hiyo kama imetengwa kimawasiliano baada ya kuendelea kwa vita dhidi ya Israel.

 ‘Bosi’ huyo wa teknolojia alitangaza kuwa atakopesha huduma zake za ‘satelaiti ya Starlink’ kwa watu wa Gaza ambayo itatoa ufikiaji wa mtandao wakati wa kukatika kwa umeme katika eneo hilo.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post