Huu ni mwaka wa tuzo kwa Billie Eilish

Huu ni mwaka wa tuzo kwa Billie Eilish

Baada ya kuondoka na Tuzo ya Wimbo Bora wa Mwaka katika Tuzo za Grammy 2024 na sasa mwanamuziki Billie Eilish, ameshinda tuzo ya wimbo bora wa mwaka katika Tuzo za Oscar 2024.

Wimbo huo uitwao ‘What Was I Made For’ ambao unasikika kwenye filamu ya ‘The Blockbuster Barbie’ kwa mwaka 2024, tayari umepata tuzo mbili kubwa nchini Marekani, ambapo mpaka kufikia sasa una zaidi ya watazamaji milioni 116, katika mtandao wa YouTube ukiwa na miezi 8 tangu kuachiwa kwake.

Billie Eilish, anatamba na ngoma zake kama ‘Lovely’, ‘Bad guy’, ‘Ocean Eyes’, ‘Bury a friend’ na nyinginezo.

Huu unakuwa wimbo wa pili kushinda Tuzo ya Wimbo Bora wa mwaka huku wimbo wa kwanza kutoka katika filamu kushinda tuzo hiyo ukiwa ni ‘My Heart Will Go On’ kutoka katika filamu ya Titanic, ulioimbwa na Celine Dion






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post