HAPA KAZI TU! Usipofanya kazi, adhabu hii itakuhusu

HAPA KAZI TU! Usipofanya kazi, adhabu hii itakuhusu

Kauli mbiu ya Rais wa awamu ya tano, Hayati John Pombe Magufuli ilikuwa ni HAPA KAZI TU!

Je ulijua kuwa usipofanya kazi ipasavyo, according to what your employer wants, utakula adhabu???

Hapa tutaelezana adhabu ambayo mwajiriwa atapewa pindi asipofanya kazi zake kwa namna ipasavyo.

Wakili Jabir anasema ni kosa kwa mwajiriwa yeyote kuzubaa na kutokufanya kazi zake kwa namna impasavyo kwa kujishughulisha na mambo yake binafsi.

Anasema adhabu ya kosa hilo ni faini au kifungo cha miezi mitatu jela au vyote kwa pamoja na hiyo ni kwa mujibu wa sheria ya makosa ya jinai na kanuni za adhabu sura ya 16.

Sasa kama wewe una mpango wa kuingia kwenye ajira, jua tu ukifika huku, CHAPA KAZI TU! Ukizubaa ovyo, itakula kwako ndugu yangu. USISEME SIKUKUAMBIA!

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm


Latest Post