Georgina ampa heshima Cr7

Georgina ampa heshima Cr7

Mpenzi wa mchezaji Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez ameonesha kum-sapoti, na kumpa heshima mpenzi wake huyo kwa kuvalia vazi lililoandikwa jina la CR7 katika maonesho ya mavazi ya ‘Vetements Fall/Winter’ yaliyofanyika usiku wa kuamkia leo jijini Paris.

Georgina alivaa gauni nyekundu yenye jina la mpenzi wake huyo pamoja na namba saba ambayo Cr7 amekuwa akiivaa toka yupo Real Madrid.

Cristiano Ronaldo na Georgina Rodriguez wapo katika uchumba kwa muda mrefu, wanaishi na watoto watano ambao baadhi yao ni watoto wa nje wa Cr7.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post