Davido kuwapeleka vijana kimataifa

Davido kuwapeleka vijana kimataifa

Mwanamuziki kutoka nchini Nigeria, #Davido amezindua lebo yake iitwayo ‘Nine+ Records’ akishirikiana na kampuni ya usambazaji wa muziki ya #UnitedMasters.

Davido ameyasema hayo kwenye moja ya mahojiano yake na #Applemusic ambapo amedai kuwa amezindua lebo hiyo kwa lengo la kuwainua wasanii chipukizi wa Afrobeat na kuwawezesha kufika level za Kimataifa.

Hivi karibuni kupitia mahujiano na podcast ya SWAY, Davido aliweka wazi kuwa muziki wa #Afrobeat umekuwa na ushindani mkubwa kwani kila mmoja amekuwa akipambana kuupeleka muziki huo ‘levo’ nyingine na kuwataja ‘mastaa’ ambao wanafanya vizuri nchini humo akiwemo #Rema, #AyraStarr na #KizzDaniel.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post