Billnass hajaibiwa, Kajizaa

Billnass hajaibiwa, Kajizaa

Kwa sasa imekuwa kama Fashion kwa baadhi ya wasanii kuonesha sura za watoto wao mara baada ya kutimiza mwaka mmoja, kama ilivyokuwa kwa #Wolper alionesha sura ya mtoto wake wa pili baada ya kutimiza mwaka moja.

#Nandy na #Billnass baada ya kuficha jina na sura ya mtoto wao wa kwanza sasa wameamua kuweka wazi sura na jina la mtoto huyo baada ya kutimiza mwaka mmoja tangu kuzaliwa kwake.

Kupitia picha za mtoto huyo baadhi ya mashabiki na watu maarufu nchini wamekuwa wakidondosha comment zao wakidai kuwa Billnass amejizaa kwani kafanana na mtoto wake, wengine wakiweka utani kuwa Billnass hajaibiwa.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post