Beyonce kufanya show Sphere 2024

Beyonce kufanya show Sphere 2024

Mfanyabiashara na mmiliki wa ukumbi maarufu kutoka nchini Marekani wa #Sphere ulioko #LasVegas, #JamesDolan inadaiwa kuwa yupo katika mazungumzo na mwanamuziki #Beyonce kwa lengo la kutaka msanii huyo afanye show katika ukumbi huo.

Ambapo madhumini ya mazungumzo hayo ni #Dolan kutaka msanii huyo atumbuiize kwenye ukumbi wa #Sphere kwa lengo la kuufanya ukumbi huo utambulike duniani kote.

Hata hivyo inadaiwa kuwa timu ya #Beyonce imetaka kiasi cha dola milioni 10 ambazo ni zaidi ya bilioni 20 za kitanzania kufanikisha msanii huyo kukubali kufanya show ndani ya ukumbi huo.

#Beyonce alimaliza ziara yake ya "Renaissance World Tour" mwezi uliyopita ambapo hajatangaza show wala ziara yoyote atakayo ifanya mwakani.

.

.

#MwananchiScoop

#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post