Abadili ndege kuwa hoteli ya kifahari

Abadili ndege kuwa hoteli ya kifahari

Mfanyabiashara maarufu kutoka nchini Urusi ambaye kwasasa anaishi China, Felix Demin (32) ameripotiwa kubadirisha ndege iliyostaafu kufanya shuguli zake za kusafirisha abiria kutoka shirika la zamani la ndege Indonesia la Mandala Air, ‘Boeing 737’ na kuwa Hotel ya kifahari

Demin alinunua ndege hiyo 2021 na kumaliza ukarabati mwanzoni mwa mwaka 2023, ndenge hiyo inadaiwa kuwa na vyumba viwili vya kulala, bwawa la kuogelea na sehemu nyingine huku ikitazamana na bahari ya Hindi.

Hata hivyo imeelezwa kuwa wateja watakaotaka kutumia nyumba hiyo kwa usiku mmoja itawagharimu takriban dola 7,300 ambayo ni zaidi ya tsh 18 milioni.

‘Boeing 737’ Hotel inapatikana katika visiwa vya Bali nchini Indeonesia.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post