Whozu: Nikiachwa tena mje mnizike

Whozu: Nikiachwa tena mje mnizike

Nyie nyie usiseme mapenzi machungu sema uliye nae hakupendi bwana, basi kupitia mitandao ya kijamii gumzo kubwa ni kuhusiana na mahusiano ya Wema na Whozu, wawili hao wanazidi kuwakera watu na kuwafunga midomo wambea wote kwa huba wanalopeana.

Kutoka katika ukurasa wa Instagram wa Whozu ameandika ujumbe ambapo umeambatana na picha za mpenzi wake madam Wema ukiwa unasema kuwa, “Ujanja sina tena ndugu zangu, nikiachwa hapa mje tu msibani,” ameandika Whozu.

Haya wanangu wa Mwananchi Scoop embu dondosha komenti yako hapo chini, Je uko tayari kufa kwa ajili ya mtoto wa mama mkwe au nikuache kidogo?






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post