Virgil kabla ya kuwa staa, alifanya kazi  mgahawani

Virgil kabla ya kuwa staa, alifanya kazi mgahawani

Beki wa ‘klabu’ ya Liverpool Virgil Van Dijk amefichua maisha aliyopitia kabla ya kuwa mchezaji mkubwa, amesema kipindi ana miaka 17 aliwahi kufanya kazi ya kuosha vyombo kwenye mgahawa.

Virgil kupitia mahojiano yake ameweka wazi kuwa kabla ya kusainiwa na ‘timu’ yoyote alikuwa akifanya kazi ya kuosha vyombo kwenye mgahawa.

Anasema licha ya kufanya kazi katika mgahawa huo hakuacha kufanya mazoezi hivyo basi akawa na ratiba ya mazoezi ambayo ni Jumatatu, Jumanne, Alhamis na Ijumaa huku siku zinazobaki alizitumia kufanya kazi hiyo.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post