Tumia vaseline kukulia nyusi na kope

Tumia vaseline kukulia nyusi na kope

Hellow Ni Friday ya kwanza ya mwaka 2022 i hope mko powa watu wangu wa nguvu, leo bwana nimekuja pambe kabisa nacho ni kukuza nyusi na kope zako kwa njia rahisi kabisa shoga anguu. 

Imekua tabia ya wanawake wengi kuweka kope za bandia lakini wakati mwingine hizi kope huleta madhara,macho kupofuka au kope kugoma kutoka.

Leo tunawaletea njia rahisi ya kukuza nyusi/kope zako, haihitaji fedha nyingi kwa sababu vitu vinavyo tumika wengi tunavyo na pia haina madhara. Faida yake kubwa ni kwamba nyusi/kope zako zinakua zako moja kwa moja kwa hivyo muonekano huu ni wa milele. 

HATUA ZA KUFUATA

  • safisha vizuri brush yako ya mascara ili kuondoa ule weusi wa mascara
  • kama ulikua umepaka make up au ume paka mafuta yoyote nawa kwa maji safi na sabuni 
  • chukua brush yako na uiweke mafuta ya vaseline
  • kisha baada ya hapo paka mafuta yako kama ambavyo unavyo pakaga maskhara
  • fanya hivi kwa muda wa wiki na utaona matokeo unaweza kuendelea kufanya mpaka pale utakapo ridhishwa na urefu wa nyusi/kope zako.

 Haya haya wadau wangu fuata tips hizo halafu uje utupe mrejesho usisahau kundondosha comment yako hapo chini @mwananchiscoop nice wikiendiii.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm


Latest Post