Travis Scott atoa bilioni 2.3 kuwasaidia wanafunzi 100

Travis Scott atoa bilioni 2.3 kuwasaidia wanafunzi 100

Rapa Travis Scott kupitia mfuko wake wa Taasisi iitwayo Cactus Jack Foundation imechangia kiasi cha Sh. Bilioni 2.3 kwa lengo la kuwafadhili kimasomo wanafunzi 100.

Ufadhili huo unakwenda kwa wanafunzi hao ambao wanahitimu 2022 katika vyuo vikuu vya watu weusi (HBCUs).

Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, Travis anahakikisha mamia ya wanafunzi kutoka vyuo hivyo vya watu weusi wanafika Diploma mwisho wa masomo yao.

Vyuo hivyo ni kama vile Texas Southern University, Alabama A&M University, Florida A&M University na vingine vingi vya watu hao.

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm


Latest Post