TMA yatoa tahadhari ya mvua kubwa

TMA yatoa tahadhari ya mvua kubwa

Taarifa ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imeeleza kuwa mvua kubwa itanyesha kwenye mikoa takribani 15 ambapo  baadhi ya maeneo ya Mikoa ya Iringa, Mbeya, Songwe, Njombe, Rukwa, Katavi, Tabora, Kigoma, Singida, Dodoma na Ruvuma yatakabiliwa na Mvua kubwa Machi 14, 2023.

Aidha , mabadiliko hayo yatasababisha Mvua kubwa Machi 15, 2023 kwenye baadhi ya maeneo ya Mikoa ya Mara, Simiyu, Shinyanga, Mwanza, Iringa, Mbeya, Songwe, Njombe, Rukwa, Katavi, Tabora, Kigoma, Singida, Dodoma na Ruvuma

Hata hivyo kwa mujibu wa TMA, athari zinazoweza kujitokeza ni baadhi ya Makazi kuzungukwa na Maji pamoja na ucheleweshwaji wa baadhi ya shughuli za Uchumi na Usafirishaji.

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Saphinia Suleiman

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, career, skills development and technology.


Latest Post