Sababu za mapenzi ya mbali kutodumu

Sababu za mapenzi ya mbali kutodumu

Eiwaaah bila shaka uko vyema kabisa wadau na wafuatiliaje wa magazine ya Mwananchi scoop leo tutaangazia suala hili hapa bwana Sababu ya mapenzi ya mbali kutodumu.

Umeshawahi kujiuliza shida inaanzia wapi?,au tatizo kubwa ni nini fuatalia dondoo hii kwa umakini ili uweze kujifunza machache ambayo unaweza ukaishi nayo.

Wengi wetu hujiuliza kwanini  maisha ya mapenzi ya mbali huwa  hayafiki mbali na kubaki wa kijiuliza tatizo ni nini? Wakati mwingine watu huanza kuulizanaa mchawi ni nani katika mapenzi yao. Laa hasha!! Huenda mchawi wa mapenzi yako ni wewe mwenyewe lakini hujui kwa sababu hakuna mtu ambaye ameshawahi kukueleza jambo hili na lile ndio tatizo.

Hata hivyo hakuna kumbukumbu ambazo zinaonesha ni kwa asilimia ngapi ambazo wapenzi wanapenda kuwa mbali mbali japo mazingira mara nyingi ndo huwa chanzo.

Katika tafiti mbali mbali zinaonesha kwamba umbali humaliza kabisa mapenzi ambayo  wapenzi wengi wenye malengo ya kufika mbali huwakuta.

Lakini zipo sababu mbalimbali ambazo ukizichanganua utajua kwa nini mapenzi mengi ya mbali huwa hayadumu

Wivu.

Adui namba moja ni huyu hapa Wivu huwa ni chachu ya kupima upendo lakini ukizidi pia huwa tatizo. Wivu wa mapenzi  ukizidi husababisha kutokuaminiana  kwani kila mmoja kwa wakati wake tofauti huhisi mwenzake anamsaliti, mara nyingi hali kama hii humfanya mmoja wapo kati ya wapenzi hao wawili kuona kama mwenzake ameshamchoka na anamtafutia sababu. Ni vyema kuwa na wivu kiasi kwa mpenzi wako

Mawasiliano

Eiwaaaah hapa napo huibua mambo kadha wa kadha Mawasiliano huimarisha mapenzi na hufanya wahusika kujihisi wapo pamoja. Inapotokea kuwa na ufinyu wa mawasiliano ndipo hali ya mapenzi ya upande mmoja hupungua na kuhisi kwamba tayari mwanamke/mwanaume tayari ameshapata mwingine wakumfanya asifanye mawasiliano ya mara kwa mara.

Ugomvi

Mmmh make hapo kwanza ncheke balaa lenyewe hutoa hapa Magomvi ya mara kwa mara hufanya mmoja wenu ahisi kuchoka na mahusiano. Inapotokea sababu za  ugomvi ambao unahisi unaweza kuwa chanzo cha kuvunja mahusiano yenu ni afadhali ukazizuia na kutafuta siku nyingine ya kutatua tatizo hilo.

Kutojali

Ukishafika level hii sasa hapo hakuna mapenzi tena, Hii mara nyingi imetajwa sana kuwa ni chanzo cha mapenzi ya mbali kuvunjika kwa sababu  tofauti mfano mpenzi wako alipokuwa karibu ulikuwa ukimpatia huduma mbalimbali kama zawadi nk, lakini anapokuwa mbali unajisahau hali hii humfanya mpenzi wako ajiulize kulikoni?

Usikivu

Nayo ni sababu ambayo ukiwauliza wengi wao ambao walikuwa na uhisiano wa mbali ukavunjika lazima atakulalamikia kwamba alikuwa hanisikilizi nachomwambia. Mfano alitaka kutoka kwenda ‘OUT’ na wenzake nikamyima lakini hajanisikiza hivyo hanifai.

Hizi huenda zikawa ni baadhi ya sababu ambazo wapenzi wengi ambao mapenzi yao hayajafanikiwa kama jinsi walivyo hitaji wamekumbana nazo.

Aloooh!! Nikukumbushe tu kuwa ili kuepuka changamoto za kutengana  na mtu ambaye unamuhitaji katika maisha yako ni vyema ukaanza kujifunza pole pole kutoka kwake ili siku ukiwa mbali naye ujue kipi mwenzako anapenda na kipi hakipendi mnapokuwa mbali.

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Saphinia Suleiman

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, career, skills development and technology.


Latest Post