Polisi ahukumiwa maisha kwa kumuua mwanaharakati

Polisi ahukumiwa maisha kwa kumuua mwanaharakati

Polisi kutoka nchini Iraq amekutwa na hatia na kuhukumiwa kifungo cha maisha kutokana na kifo cha mchambuzi mashuhuri wa masuala ya usalama na mkosoaji wa mara kwa mara wa wanamgambo wenye nguvu.

Hukumu hiyo iliyotolewa jana siku ya Jumapili, katika kipindi cha  karibu miaka mitatu baada ya mchambuzi huyo kupigwa risasi nje ya nyumba yake Baghdad kufuatia vitisho vya wanamgambo.

Familia ya marehemu, Hisham al-Hashimi, imeonesha kufurahishwa na uamuzi huo lakini pia imeonesha wasiwasi kwamba uenda ikabatilishwa na kukatiwa rufaa.

Aidha Al-Hashimi aliyekuwa na umri wa miaka  47, aliuawa kwa kupigwa risasi Julai 2020 mbele ya nyumba yake huko Baghdad na washambuliaji wawili waliokuwa kwenye pikipiki baada ya kupewa vitisho kutoka wanamgambo wanaoungwa mkono na Iran.

Chanzo DW






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post